Numbers 32:20-22

20 aKisha Musa akawaambia, “Kama mtafanya jambo hili, kama mtajivika silaha mbele za Bwana kwa ajili ya vita, 21na kama ninyi nyote mtakwenda mmejivika silaha ng’ambo ya Yordani mbele za Bwana mpaka awe amewafukuza adui zake mbele zake, 22 bhadi wakati nchi itakapokuwa imeshindwa mbele za Bwana, ndipo mtaweza kurudi na kuwa huru kutoka masharti yenu kwa Bwana na Israeli. Nayo nchi hii itakuwa milki yenu mbele za Bwana.

Copyright information for SwhKC